
Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Mussa Uledi alisema
hayo wakati akifunga maonesho ya 39 ya biashara na kusema kuunganishwa
huko kumefanyika katika mikutano ya kibiashara kwa washiriki wa maonesho
hayo.
Alisema mazungumzo hayo ya kibiashara yafuatiliwe kwa kushirikiana na sekta binafsi ili yazae matunda.
Uledi alisema maonesho ya mwaka huu yamefana kutokana na maandalizi
mazuri, bidhaa zenye ubora wa hali ya juu zilizotokana na ubunifu mkubwa
kwa wazalishaji, utangazaji wa bidhaa na wataalamu wa masoko wenye
kutoa maelezo fasaha kuhusu bidhaa na huduma zao.
Alisema amepata faraja kuwa na mabanda maalumu ya bidhaa za aTanzania
kwa ajili ya kutangaza bidhaa za nchini, banda la asalina lile la elimu
na kutoa ushauri wa kubainisha bidhaa zingine ili nazo zitafutiwe
mabanda maalum ili zionekane na kutangazwa kwa lengo la kutafuta masoko.
Alisema serikali itaendelea kutoa ushirikiano ili maonesho hayo
yaendelee kuwa na kiwango cha kimataifa kwani mafanikio ya maonesho hayo
yanahitaji ushirikiano wa serikali na wazalishaji wa bidhaa na
watumiaji.
Mkurugenzi wa TANTRADE, Jacqueline Maleko aliwashukuru washiriki wote
na kuwakaribisha katika maonesho ya mwakani aliyoahidi kuwa bora zaidi.
No comments:
Post a Comment